Friday, June 20, 2014

WIZARA ya mambo ya ndani yakiri askari wa jeshi la polisi na magereza kukosa makazi yanayoridhisha


Naibu waziri wa mambo ya ndani Pereira Ame Silima akiongea bungeni mjini Dodoma

SERIKALI imekiri kuwa baadhi ya askari polisi na hata wa magereza , Hawana makazi yanayoridhisha hatua inayosababisha wazazi kukosa faragha wanayohitaji katika jamii.
Naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi PEREIRA AME SILIMA, amesema hayo jana bungeni mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la mbunge wa viti maalumu, SUZAN LYIMO kupitia chama cha chadema katika swali lake lililosema askari polisi Nchi nzima wanashida ya makazi ambayo imesababisha hata faragha ya wazazi kukosekana kwa kuwa wanashirikiana chumba kimoja na watoto.
Akifafanua juhudi za serikali za kukabiliana na hali hiyo SILIMA amesema tatizo hilo si la polisi pekee bali hata askari wa magereza lakini serikali imeanza kujenga ghorofa sehemu mablimbali Nchini ili familia hizo zipate nafasi zaidi.
Kwa mujibu wa Silima pia jeshi la polisi limeanziasha shirika litakalokuwa na kazi maalumu ya kushughulikia makazi ya askari  ili kazi hiyo iwe endelevu na hatimaye changamoto hiyo iishe.
Awali katika swali la msingi mbunge wa mbogwe Augustino Masele amesema kuna malalamiko kuwa wakuu wa polisi wa wilaya wamekuwa wakikosa mafuta kwa ajili ya utendaji kazi wa kila siku ambapo  akaitaka serikali itoe ahadi ni lini itaanza kupeleka fedha hizo za mafuta moja kwa moja kwa wakuu wa polisi badala ya kupitisha kwa makamanda wa polisi wa Mkoa .



No comments:

Post a Comment