Friday, June 20, 2014

DIWANI mstaafu wa Mkwatani, Kilosa afariki dunia

Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Morogoro Innocent  Kalogeresi

ALIYEKUWA  Diwani Mstaafu wa kata ya Mkwatani wilayani Kilosa Mkoani Morogoro kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Amina Mwarabu amefariki ghafla nyumbani kwake alfajiri ya june 19 mwaka huu.
Akizungumza na Mbiu ya Maendeleo mjini Kilosa, mtoto mkubwa wa marehemu,Bwana   Ally  Nassoro  amesema kuwa mama yake alikuwa na maradhi ya moyo na kisukari ambayo yalikuwa yakimsumbua kwa muda mrefu na alikuwa anaendelea kutumia dawa hali inayosadikika kuwa imesababisha kifo hicho.
Aidha Nassoro ameongeza kwa kusema kuwa marehemu mama yake amefariki akiwa na umri wa miaka 62 na ameacha jumla ya watoto wane wakiwemo wa kiume watatu na wa kike mmoja.
Akiongeza kwa niaba ya chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilosa katibu Msaidizi Twaribu Kassimu Kaberege amesema kuwa msiba huo wameupokea kwa masikitiko makubwa kwani marehemu alikuwa Mwenyekiti mstaafu wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Kilosa na pia alikuwa makamu mwenyekiti msaidizi wa Baraza la Wazee Wilaya ya Kilosa.
Kaberege amesisitiza kwa kusema kuwa hilo limekuwa pengo kubwa kwa jamii ya Kilosa na Taifa kwa ujumla kwani marehemu alikuwa mstari wa mbele katika kupigania maendeleo ya watanzania.


No comments:

Post a Comment