![]() |
| Jaji mstaafu Damiani Lubuva akiongea na waandishi wa habari |
MWENYEKITI
wa Tume ya uchaguzi (NEC) Jaji mstaafu DAMIANI LBUVA amesema kuwa vitambulisho
vya kupiga kura nchini vitatolewa upya kwa wananchi wote ikiwa ni sehemu ya
mchakato wa kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura.
Ameyasema
hayo hivi karibuni wakati akifungua mkutano kati ya tume na wahariri wa vyombo
mbalimbali vya habari kuhusu uboreshwaji wa daftari la wapiga kura.
Jaji
LUBUVA ameeleza kuwa mchakato huo wa kutoa vitambulisho upya utakaotekelezwa
septemba mwaka huu utagharimu sh bilioni 293 Tofauti na vitambulisho vyaawali
vya karatasi vilivyotolewa kwa mara ya kwanza mwaka 2004 kutokana na matumizi
ya teknolojia mpya katika uandikishaji.
Ameongeza
kuwa katika uboreshaji huo wapiga kura wa zaman kwa maana waliokuwa kwenye
daftari la sasa watatakiwa kwenda katika vituo vya kujiandikisha kuchukuliwa
taarifa zao hasa alama za vidole picha na saini zao katika mfumo mpya wa BVR na
hatimaye kupewa vitambulisho vipya.
Aidha
Jaji LUBUVA amesema vitambulisho hivyo vipya vitatolewa papo hapo uandikishaji
ukikamilika na vitakuwa vya plastiki ngumu na namba ya mpiga kura.

No comments:
Post a Comment