Wednesday, June 18, 2014

WATOTO milioni 30 hawaendi shule Afrika


 
Watoto nchini jamhuri ya Afrika ya kati(CAR)


MASHIRIKA mawaili ya Umoja wa Mataifa yamesema kuwa, karibu watoto milioni 30 wa shule za msingi hawaendi shule barani Afrika  kutokana na umasikini na migogoro
.Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa  (UNICEF) na  Shirika la Umoja wa Mtaifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) yamesema kuwa, watoto milioni 19 hawaendi shule huko magharibi na katikati mwa Afrika na wengine milioni 10 hawahudhurii shuleni katika maeneo ya kusini na mashariki mwa bara hilo.

Ripoti za mashiria hayo zimeeleza kuwa, matatizo ya fedha yanayoisumbua dunia nzima na machafuko katika bara la Afrika pia vimekwamisha jitihada za kuwarejesha watoto shuleni.

Yumiko Yokozeki, mshauri wa elimu wa UNICEF amesema, shule nyingi zimefungwa katika nchi zenye machafuko za Jamhuri ya Afrika ya Kati, Nigeria na Mali.

No comments:

Post a Comment