Saturday, June 21, 2014

JAMII yatakiwa kuwafichua wafanyabiashara wa vipodozi vilivyopigwa marufuku


Afisa wa Mamlaka ya chakula na dawa nchini( TFDA) akiongea na wanahabari

MAMLAKA ya chakula na dawa nchini (TFDA) imeitaka jamii ya watanzania kuwafichua watu wanaofanya biashara ya vipodozi visivyoruhusiwa na serikali kwa kuwaripoti nkatika ofisi za mamlaka hiyo.


Wakiongea  na Mbiu ya Maendeleo katika viwanja vya Mnazi  mmoja jijini Dar es salaama katika maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja hivyo watumishi mamlaka hiyo wamesema kuwa mapambano dhidi ya vipodozi haramu yatafanikiwa endapo wananchi watashiriki kikamilifua katika kuwafichua wafanyabiashara wanaokiuka taratibu za uagizaji na uingizaji wa vipodozi vuisivyoruhusiwa.

Wamesema, kwa mujibu wa tafiti walizozifanyaimebainika kuwa  wafanyabiashara wa vipodozi vilivyopigwa marufuku ni watu wenye historia ya kufanya makosa makubwa ya uhalifu hivyo ni vyema mapambano hayo yakashirikikisha kila mdau .

 Mbali na Vipodozi Mamlaka hiyo inashughulikia uuzaji wa bidha zilizokosa viwango na kuisha muda wake.

No comments:

Post a Comment