Friday, June 27, 2014

ASILIMIA 3.5 wakutwa na maambukizi ya ukimwi katika sherehe za mwenge, wilayani Kilosa


Mkuu wa wilaya ya Kilosa Elias Tarimo

ZAIDI  ya wakazi mia mbili waliokesha kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru juni 23 mwaka huu katika Kata ya Kisanga Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro ni asilimia 3.5 ndiyo waliokutwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI na vimelea vya ugonjwa wa malaria

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Elias Tarimo kabla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru ngazi ya Mkoa mara baada ya kumaliza mkesha Kata ya Kisanga juni 24 mwaka huu, pia amesema katika tathimini hiyo iliyotolewa ni kwa sababu ya mwitikio chanya kwa wananchi kujitokeza kupima kwa hiari .
Aidha Tarimo amesema kuwa jumla ya waliojitokeza kupima virusi vya UKIMWI ni 325 tu ambapo wanaume 182 na wanawake 143, huku wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI ni 8 wanaume 3 na wanawake 5 ambayo ni sawa na asilimia 2.5, pia waliopima malaria 287 wanawake 138 wanaume 149 waliokutwa na vimelea vya malaria ni 30 sawa na asilimia 1.1 na wamepatiwa maelekezo sahihi ya kutumia dawa za malaria na kisha kukabidhi Mwenge kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
Hata hivyo Mkuu wa MKoa wa Morogoro Joel Bendera amesema kuwa ameupokea Mwenge ukiwa salama na ameukabidhi   mkoa wa Iringa kwa Mkuu wa Mkoa Christine Ishengoma na amewasisitiza wananchi kuzingatia ujumbe wa Mwenge usemao Katiba ni sheria kuu ya nchi chini ya kauli mbiu isemayo Jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya.
Ameongeza kwa kusema kuwa wananchi wanapaswa kuacha kufanya marumbano yasiyo na msingi hali ambayo itazorotesha maendeleo ya jamii pia kutumia vyandarua vyenye dawa ili kufikia lengo la Tanzania bila malaria inawezekana na mara ujihisipo na dalili za malaria wahi kituo cha Afya ukapate huduma na Tanzania bila UKIMWI inawezekana jitokeze kupima kwa hiari ili kutokomeza maabukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

No comments:

Post a Comment