![]() |
| Mipaka ya nchi za maziwa makuu |
WACHUNGUZI kutoka
jumuiya ya mataifa ya eneo la maziwa makuu wamechapisha ripoti kuhusu mapigano
ya hivi karibuni yaliyotokea katika eneo la mpaka kati ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo na Rwanda.
Ripoti
hiyo inasema kuwa mapigano hayo yalitokana na mzozo wa ardhi kati ya mataifa
hayo mawili katika maeneo ya milima miwili jirani.
Hata
hivyo ripoti hiyo inasema kuwa mapigano ya hivi majuzi yanatokana na kutokuwepo
mpaka kamili kati ya mataifa hayo mawili.
Katika
mapigano hayo ya hivi karibuni mataifa hayo yalikuwa yakigombania milima miwili
ambayo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilidai yote ni yake huku Rwanda ikisema
inamiliki mlima mmoja.

No comments:
Post a Comment