Monday, June 23, 2014

UFARANSA yakiri kuwa hali ya mambo Afrika ya kati ni mbaya


Wanajeshi wa Ufaransa nchini Afrika ya kati(CAR)

HALI ya mambo ya Jamhuri ya Afrika ya Kati bado ni mbaya licha ya kuweko maelfu ya wanajeshi wa Ufaransa nchini humo.


Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa  Jean Yves Le, amesema kuwa hali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati hairidhishi,hivyo juhudi kubwa zinapasa kufanywa ili kutafuta suluhisho la mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.

 Amesema kuwa viongozi wa kisiasa wa nchi za Kiafrika wanajukumu la kuchangia jitihada za kutafuta suluhisho la mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati. 

Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa amewapongeza pia wanajeshi 2000 wa nchi yake ambao walitumwa Jamhuri ya Afrika ya Kati tangu mwezi Disemba mwaka jana.
 
Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa anavipongeza vikosi vya nchi yake vilivyopo Jamhuri ya Afrika ya Kati katika hali ambayo duru za habari za Ufaransa siku kadhaa zilizopita ziliutathmini utendaji wa miezi sita wa vikosi vya Ufaransa huko Jamhuri ya Afrika ya Kati kuwa ni dhaifu san

No comments:

Post a Comment