![]() |
| Bi Meriam Ibrahimu aliyehukumiwa kifungo nchini Sudan |
MWANAMKE aliyehukumiwa
kifo nchini Sudan Bi Merian Ibrahimu akiwa amejifungua mtoto akiwa
kizuizini huenda akaachiwa huru siku
chache zijazo
.
Ripoti zilizotolewa mwishoni mwa
wiki ziliarifu kwamba afisa mmoja wa
serikali alithibitisha Meriam Ibrahim, aliyejifungua mtoto akiwa kizuizini
ataachiliwa katika siku chache zijazo.
Lakini wizara ya mambo ya nchi hiyo
imesema kuwa Bint Ibrahim anaweza tu
kuachiliwa ikiwa kesi yake ya rufaa itafanikiwa.
Bi Meriam Ibrahim, alilelewa na mama aliyekuwa
mkristo , lakini mahakama ilimhukumu kifo ikisema kuwa anapaswa kuwa muisilamu,
hiyo ndiyo iliyokuwa dini ya babake.
Alikataa kusilimu na kusema kuwa yeye ni mkristo na hivyo anakabiliwa na hukumu ya kunyongwa kwa kosa la kuasi dini.
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Sudan, Abdullahi al-Azreg, aliwaambia waandishi wa habari kuwa , Bint Ibahim ataachiliwa huru kwani serikali ya Sudan inawapa watu uhuru wa kuabudu na hivyo iko tayari kumlinda.
Mumewe Meriam Daniel Wami, alisema kuwa taarifa za mkewe kuachiliwa ambazo amezisikia kupitia vyombo vya habari, ni kama uvumi tu.

No comments:
Post a Comment