![]() |
| Dk Mary Mgonja akiwa katika shamba la mtama mkoani Singida |
HATIMAE dawa ya kukomesha Mawakala
wabadhilifu wa pembejeo nchini imekamilika kwa kutungwa sheria ya pembejeo
itakayo komesha kabisha uchakachuaji na wizi kupitia pembejeo nchini
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi msaidizi kitengo cha usambazaji wa pembejeo za kilimo kutoka wizara ya kilimo na ushirika Kanuti Komba wakati akizindua nembo ya chama cha mawakala wa mbegu nchini (TANADA) na kuwasisitiza kuacha tabia hiyo vinginevyo watafilisika na kuishia jela.
Katika uzinduzi huo uliowakutanisha
mawakala hao kupitia wawakilishi na wajumbe toka kanda ya Ziwa,Magharibi,
kati,kusini na Kasikazini,Komba alisema serikali imechoshwa na kelele zisizo na
tija juu ya hujuma zinazofanywa na mawakala hao kwa wakulima.
Akithibitisha kuwa biashara ya
pembejeo 'inalipa'kwa mfanya biashara alionyesha kushangazwa na baadhi yao
kuharibu dhana ya serikali kumwezesha mkulima ili azalishe zaidi kwa
kuwachakachulia na kuwaibia ili wajinufaishe zaidi.
Kwa upande wake wakilishi wa
Alliance for Green Revolutin in Africa (AGRA) ambao ni wafadhili wa
mawakala wa pembejeo za kilimo nchini Dk Mary Mgonja alisema shirika hilo
limeamua kuwafadhili mawakala hao baada ya wakulima hao kuwa na tatizo la
usambazaji wapembejeo vijijini.
Alisema AGRA imejipanga
kikamilifu kuhakikisha linafadhili kila kanda kwa lengo la kutoa
elimu ya usambazaji wa
pembejeo kwa lengo la kukuhakikisha wakulima wanapata pembejeo kwa wakati.
Awali mwenyekiti wataifa TANADA Michael Mahicha na
mwenyekiti wa TANADA Mkoa wa Morogoro Amini Lubegete walimwambia mgeni
rasmi kuwa wameanzisha chama hicho kwa lengo la kusaidia serikali inafanikisha
malengo yake kupitia kilimo kwa kugawa pembejeo kwa njia sahihi hasa vijiji.
walisema wameamua
kufanya hivyo ili iwarahisishia kuwabaini na kuwabana wenye tabia mbaya ya
kujinufaisha kwa kutoa huduma duni kwa wakulima ambapo pia wanakusudia
kuanzisha chama cha kuweka na kukopa SACCOS ili kuwezeshana kufikia lengo la
taifa.
Aidha waliiomba serikali
kushirikiana na naokuweka mkakati kuwadhibiti wasambaza pembejeo feki kwa njia
mbalimbali ikiwemo ya kushitakiwa na kufutiwe leseni zao maisha.

No comments:
Post a Comment