Monday, June 23, 2014

HALMASHAURI ya wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro yapongezwa kwa kupata hati safi


Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera 

MKUU wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Kilombero kwa hati safi katika miaka mitatu mfululizo na kuzitaka halmashauri nyingene tano zilizobaki katika mkoa huo kujifunza wilayani Kilombero
.

Akizungumza kwenye baraza maalumu la madiwani wilayani humo Bendera alisema kuwa juhudi zinazofanywa na halmashauri hiyo ni hazina tosha ya maendeleo ya mkoa hivyo halmashauri zilizobaki hazina budi kuiga maramoja ufanisi wake.


Hata hivyo mkuu huyo alishangazwa na baadhi ya kuendekeza mikopo hewa,uwasilishaji taarifa zisizo kiwango cha kimataifa,michanganuo isiyoeleweka kwenye mapato na matumizi na halmashauri kutorejesha asilimia 20 ya mapato kwenye vijiji.

Kwa upande wake mkaguzi mkazi wa Morogoro Silvester Kibona hoja za nyuma za halmashauri hiyo zilikuwa 97 lakini hivi sasa zimetekelezwa hoja 90 na zimebaki 7 na hizo zilizobaki zinahitajika zitoke kabisa.

Awali mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Azimina Mbilinyi alisema mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG alilazimika kutoa hati safi kwenye halamashauri hiyo baada ya kulidhiswa na ubora wa hesabu za kwa mwaka wa fedha 2012/2013  

No comments:

Post a Comment