Wednesday, June 18, 2014

Cuf Kilosa waahirisha uchaguzi kutokana na idadi ya wajumbe kutokamilika



 
Mwenyekiti wa CUF Taifa Prof Ibrahimu Lipumba
MKUTANO Mkuu wa Uchaguzi wa Chama cha Wananchi( CUF) Wilayani  Kilosa Mkoani Morogoro uliokuwa ufanyike juni 15 mwaka huu umehairishwa kutokana na sababu mbalimbali hadi utakapotajwa tena na Uongozi wa Wilaya.


Hali hiyo imejidhihirisha katika Ukumbi wa Manyovu uliopo Wilayani Kilosa ambapo ndipo Uchaguzi ulipangwa kufanyika saa mbili usiku  ili kuweza kuchagua Viongozi mbalimbali wa Wilaya mara baada ya kushindwa kuhudhuria robo tatu ya wajumbe wa Chama hicho.
Kwa mujibu  wa Mjumbe wa Uchaguzi ngazi ya Taifa Husein Shaban Mwakikoti amesema kuwa mkutano huo ulikusudiwa kuwa na wajumbe mia tatu lakini hadi kufikia saa tano usiku wajumbe mia moja na ishirini tu ndio waliokuwa wamewasili,hali iliyosababisha kuahirishwa kwa uchaguzi  kwa mujibu  wa Katiba ya chama hicho inayosema kuwa Uchaguzi utafanyika kama kutakuwa na  nusu ya wajumbe wote

No comments:

Post a Comment