Wednesday, June 18, 2014

WANAFUNZI wapigwa marufuku kujishughulisha na biashara yoyote pindi wawapo shuleni





Mkuu wa wilaya ya Kilosa Eliasi Tarimo
MKUU  wa wilaya ya Kilosa Elias Tarimo amepiga marufuku wanafunzi kujishughulisha na biashara yoyote pindi wawapo shuleni na nyumbani ili kutimiza Sera ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto.


Tarimo ameyasema hayo Juni 16 mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika Kiwilaya katika Kata ya Zombo  kijiji cha Nyali na kusema kuwa ni marufuku kwa wazazi kuwatuma watoto kufanya biashara yoyote ile kwani ni kinyume na sheria.

Aidha Tarimo amesema kuwa wazazi wanawajibu wa kuhakikisha watoto wao wanapata mahitaji yote muhimu shuleni kama vile madaftari na sare za shule ili kujenga mazingira rafiki ya kusoma na kujifunza ili kutekeleza mpango wa Serikali wa matokeo Makubwa Sasa(B.R.N) kwani Elimu ndiyo chachu ya Maendeleo.

Sambamba na hayo amewaasa wazazi kuwapeleka watoto shule kwa kipindi muafaka na kuhakikisha mtoto anakuwa shuleni muda wote wa masomo kwani kila mtoto ana haki ya kupata Elimu bila kujali jinsia wala ulemavu

No comments:

Post a Comment