Issa Timamy hata hivyo hatakiwi
kujibu mashtaka hayo wakati huu.
Timamy alikamatwa Jumatano jioni na
maafisa wa polisi na kuhojiwa kabla ya kuzuiliwa usiku katika kituo kimoja cha
polisi. Alifikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Aidha Timamy anakuwa mwanasiasa wa
kwanza wa ngazi ya juu kushtakiwa kuhusiana na mauaji hayo, ambayo ni mabaya
zaidi tangu yale yaliyotokea katika eneo la Westgate Jijini Nairobi.

No comments:
Post a Comment