![]() |
| Katibu mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue |
MAADHIMISHO ya wiki ya
Utumishi wa umma yanatarajiwa kugfungwa
kesho jioni baada ya takribani wiki moja ya kuonesha wananchi shughuli
mbalimbali zinazofanywa na Taasisi mbalimbali za wizara hapa nchini.
Akiongea na Mbiu ya Maendeleo mapema
leo katika viwanja vya Mnazi mmoja ,jijini Dar es salaam,Muwezeshaji toka
wizara ya maliasili na Utalii amesema kuwa , wananchi wamejifunza mengi toka
katika banda la wizara hiyo yenye jukumu la kutunza maliasili za
Taifa ikiwa
nipamoja na kupata maelezo ya namana ya kupambana na ujangili wa maliasili hasa
meno ya Tembo.
Amesema, kwa wananchi
wanaohitaji kupata mengi kuhusu majukumu na kazi mbalimbali za wizara hiyo
wanakaribishwa kwenye maonesho ya sabasaba yanayotarajiwa kuanza tarehe 28,juni
2014 siku ya jumamosi na kumalizika tarehe08,kwa kuwa wanatarajia kushirikia
kwenye maonesho hayo.
Mgeni rasmi wa kufunga wiki ya madhimisho ya wiki ya Utumishi wa umma anatarajiwa kuwa Katibu mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

No comments:
Post a Comment