WAZIRIwa mambo ya nje nchini Marekani John Kerry amewasili nchini Misri kwa lengo las kukutana na rais
mpya wa Misri Abdul Fatah Al Sisi.
Waziri huyo wa Marekani ndiye kiongozi wa kwanza kutembele nchi ya Misri tangu kamanda huyo wa zamani wa jeshi
kuchaguliwa kama rais baada ya kumpindua aliyekuwa rais wa Taifa hilo Mohammed
Morsi.Maafisa wa Marekani wanasema kuwa lengo kuu la bwana Kerry kuzuru nchi hiyo ni kumtaka rais Abdul fatah Al sisi kuwashirikisha watu wote katika siasa yake ikiwemo wanachama wa kundi la Muslim Brotherhhood lililopigwa marufuku.
Kerry pia anatarajiwa kuzungumzia kuhusu hukumu ya kifo iliotolewa dhidi ya wanachama wengi wa kundi hilo mbali na kutoa wito wa kuachiliwa kwa waandishi waliofungwa.
Kwa mujibu wa vyombo vvya habari vilivyoongozana na kiongozi huyo wa Marekani vinasema kuwa, bwana kerry amesema kuwa Marekani iko tayari kuanzisha mazungumzo na rais huyo mpya ikiwa na matumaini kwamba mazungumzo hayo yataleta natija.

No comments:
Post a Comment