Monday, June 30, 2014

VIONGOZI wa vyama vya siasawatakiwa kuwashirikisha wazee katika shughuli za vyama

Wazee wilayani  Kilosa



VIONGOZI wa vyama vya siasa wilayani Kilosa,mkoani Morogoro wametakiwa kuwashirikisha wazee kwenye shughuli zao mbalimbali za vyama vyao ili kuwaenzi wakitambua kuwa mzee ni muhimu wakati wowote si wakati tu wa nyakati za uchaguzi .


Hayo yamesema hivi karibuni katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilosa kwenye mkutano wa wadau na wajumbe wa Baraza la wazee wilaya na wazee wa Baraza hilo.
Wazee hao wameeleza kuwa viongozi wa vyama vya siasa wanapaswa kuwathamini na 

kuwatumia wazee wakati wote wa shughuli zao mbalimbali za vyama vyao wasisubirie mpaka  kipindi tu cha uchaguzi wakiwaona kuwa ndio bora zaidi ili wawapigie  kura.

Akizungumzia hilo katika sera zao vyama vyao katibu wa chama cha CUF wilaya ya Kilosa Sudi Momborage , Mwenyekiti  wa chama UDP Maarufu  Salehe Mkambala na mwenyekiti wa NCCR Magenzi Salumu Mtupe  wameeleza kuwa sera za vyama vyao vinawatahamini wazee na ikiwemo ushirikiano katika haki sawa  kuwaunganisha pamoja ili waweze kutambulika kama makundi mengine .

Naye katibu wa chama cha mapinduzi CCM wilayani Kilosa Dodo Samba amesema sera ya Iran ya chama cha mapinduzi.


No comments:

Post a Comment