NAIBUMKURUGENZI
wa Mtandao wa jinsia Tanzania TGNP Lilian Liundi amewataka wanawake nchini
kuijua bajeti ya nchi kisera na kisekta kisha kuwa mstari wa mbele kuifuatilia
ili iwasaidie kutathimini na mafanikio yake kwao.
Mbali na hilo pia ameishauri jamii
kuzielewa vema sera za kisekta nchini ili kuwapa uwezo wa kuhoji baada ya
kutambua mafanikio na changamoto zake katika upatikanaji wa maendeleo kupitia
bajeti zilizopo.
Akifungua mafunzo wanawake ngazi ya
jamii na waandishi wa habari katika ofisi za mtandao huo,Lilian alisema bajeti
nyingi hazifikii malengo yake katika utekelezaji kutokana na uelewa mdogo juu
ya bajeti hizo sambamba na umuhimu wake katika maisha ya kila siku katika
jamii.
Awali mkuu wa Taasisi ya mafunzo
katika mtandao huo Ziki Mihyo aliwataka watanzania hususani wanawake
kutengeneza mkakati wa ushawishi na utetezi katika masuala ya bajeti katika
maeneo walipo ili utekelezwaji wake uende sambamba na matakwa ya sera na
mahitaji ya jamii.
.
Jumla ya wanawake,waandishi wa
habari 35 kutoka vituo na vyombo mbalimbali vya habari nchini wapo jijini Dar
es salaam katika mafunzo ya utambuzi wa bajeti na ushiriki wake katika
kujiletea maendeleo ya kiuchumi kwenye jamii na taifa kwa jumla.

No comments:
Post a Comment