Monday, June 30, 2014

WASANII MORO wamuomba Rais Kikwete kuwajengea kituo cha redio na runuinga


Mkuu  wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera

WASANII  mkoani Morogoro wamemuomba Rais Jakaya Kikwete kumalizia muda wake wa utawala nchini kuikuza tasinia ya sanaa kwa kuwajengea kituo maalumu cha redio na televisheni itakayokuwa na kazi ya kuibua vipaji,kutangaza na kuonyesha kazi za wasanii tanzani.


Ombi hilo mbele ya Mkuu wa mkoa huo Dk.Joel Bendera katika utoaji tuzo ya vipaji ‘Moro town talent award’ na uzinduzi wa jingo la kuandalia kazi mbalimbali za wasanii ‘Moro Town Records’ lilikwenda sambamba na ombo la mkoa huo kuwa kitovu cha usanii nchini kutokana na historia yake katika tasinia hiyo.

Mbele ya mkuu huyo aliyewakilishwa na Afisa tarafa ya Manispaa Pakala pakala Mulenge,Mkurugenzi  wa kituo hicho na mwenyekiti wa wasanii mkoani humo Mohamed Ngwenje alisema kilio cha wasanii kupata vituo vya habari ni kuikuza haraka tasinia hiyo na kuepuka changamoto zilizo kwenye vyombo vya habari.

 Akijibu madai hayo kwa niaba ya Mkuu wa mkoa,Pakalapakala alisema wazo la wasanii hao ni zuri na linalenga kukabili bomu la ajira kwa vijana na serikali kwa kadri ya uwezo wake itajitahidi kulitafutia ufumbuzi.

Katika uzinduzi huo waandishi wa habari,vyombo vya habari,wasanii katika fani mbalimbali,watu binafsi,taasisi,mashirika na makampuni walitunukiwa tuzo ya umahili katika sekta yake na Moro Talent award.


WAKULIMA  wa zao la mhogo wilayani Kisarawe ,mkoa wa Pwani  washukuru mwezi mtukufu wa ramadhani kutokana na kuongezeka kwa mauzo ya zao hilo.

Wakiongea na Mbiu ya Maendeleo wilayani  hapo , wakulima hao wamesema kuwa, kweli mwezi wa ramadahani ni neema kimwili na kiroho kwani tunashukuru toka  jana kumekuwa na ongezeko kubw ala mazuo ya muhogo kutokana bna wafanyabiashara wengi toka jijini Dar kuja kwa wingi katika vijiji mbalimbali vinavyozalisha muhogo wilayani Kisarawe.

Hata hivyo  wamesema , ni vyema serikali ikawasaidia namna bora ya usindikaji wa zao hilo ili kuoingeza thamani kutakoendana na ukuzaji wa uchumi wa mkulima mdogo.  






No comments:

Post a Comment