Wednesday, June 4, 2014

WATANZANIA wataungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya mazingira dunia inayofanyika juni 5 kila mwaka


KESHO ni maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambapo kitaifa yatafanyika jijini Mwanza ambapo kutapambwa na shughuli mbalimbali za usafi wa mazingira ikiwemo kusafisha maeneo , kuzoa taka,kupanda miti inayofaa n.k


 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na waziri ofisi ya makamu  wa Raisi (mazingira) Dk Binilith S. Mahenge kwa vyombo vya habari nchini, watanzania tutaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya mazingira duniani ambayo hufanyika  juni 5, kila mwaka .

Waziri Mahenge wamewataka watanzania kutunza mazingira  na kutoachoma moto hovyo ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo  ynakuja kwa kasi kubwa nchini na duniani kwa ujumla .

Kwa mujibu wa taarifa ya tano ya jopo la wataalamu wa kimataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, sekta ya nishati inachangia asilimia 25,sekta ya kilimo, misitu na matumizi ya ardhi inachangia   asilimia 24,viwanda 21 usafirishaji asilimia 14 na sekta nyingine asilimia 9.6 shughuli hizi ndizo chanzo cha ongezeko la gesijoto duniani.

No comments:

Post a Comment