Thursday, October 23, 2014

WANANCHI wahamasishwa kujiunga na vikundi vya uzalishaji mali


Abdulsalam Sas (katikati) na Mohamed Abdul azizi (kulia|)

MBUNGE wa jimbo la Mikumi Abdulsalam Ameri  Sas amewataka wananchi jimboni humo kuacha kujipatia kipato kwa njia haramu ikiwemo ya kujihusisha na ujangaili badala yake wajikite zaidi katika ubunifu ikiwemo kuunda vikundi vya uzalishaji kama kuweka na kukopeshana fedha.

Sas alisema hayo wakati akizindua tamasha la Ujirani Mwema la kupinga ujangili kwa wanyama waliohatarini kutoweka wakiwemo Tembo,Faru na Twiga lililoandaliwa na  Mtandao wa habari za  kijamii Tanzania ( MHAKITA).
Aliwataka wananchi hao kuunda vikundi vya ujasiliamali vitakavyowasaidia kujikwamua kiuchumi na sio kutegemea kuhujumu rasilimali za
nchi hasa mazo ya misitu.

No comments:

Post a Comment