Tuesday, January 27, 2015

CHIKAWE alitaka jeshi la polisi nchini kupanga mikakati kudhibiti uhalifu



Waziri wa mambo ya ndani Mathias Chikawe

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametahadharisha juu ya kuongezeka kwa mitandao ya uhalifu wa kimataifa na ugaidi.

Kutokana na hali hiyo waziri Chikawe amesema kuwa , kama haitadhibitiwa mapema na vyombo vya dola, inaweza kujipenyeza katika sekta mbalimbali ikiwamo kufadhili watafuta uongozi wa nchi.
Mathias Chikawe amelitaka Jeshi la Polisi nchini Tanzania kupanga mikakati thabiti ya kuhakikisha amani na utulivu uliopo nchini  unaendelea kuimarishwa hasa wakati wa kampeni na upigaji kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa. Amesema,.
Uhalifu wa kimataifa hutumia fedha chafu zinazopatikana kwa njia haramu na kuwa ni hatari kwa usalama wa taifa kutokana na kwamba kutokana na uwezo mkubwa wa kifedha wa mitandao hiyo, ni rahisi kujipenyeza hata katika uongozi. Kuhusu kuibuka kwa makundi ya kihalifu kama vile 'Panya road', Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Tanzania amesema, hali hiyo haikubaliki na kulitaka Jeshi hilo kutimiza wajibu badala ya kusubiri matukio yatokee.

No comments:

Post a Comment