Tuesday, January 27, 2015

UMOJA wa Afrika wataka hatua za dharula kuchukuliwa kudhibiti boko Haramu


                  Bi. Nkosazana Dlamini-Zuma

UMOJA wa Afrika AU umesisitiza juu ya kuweko udharura wa kuchukuliwa hatua za pamoja za kukabiliana na kundi la kigaidi la Boko Haram la nchini Nigeria.

 Taarifa ya Umoja wa Afrika imezitaka nchi wanachama wa umoja huo kuchukua hatua za maana na za pamoja za kupambana na kundi la Boko Haram ambalo limehatarisha usalama wa Nigeria na nchi jirani na nchi hiyo.
Mkutano wa Umoja wa Afrika ulianza jana katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa ajenda kuu zikiwa ugonjwa wa Ebola na Boko Haram. Akihutubia katika kikao cha ufunguzi wa mkutano huo, Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika,  amezitaka nchi wanachama wa AU kuchukua hatua za pamoja za kukabiliana na tishio la Boko Haram. Kwa upande wake Carlos Lopez Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiuchumi ya Umoja wa Mataifa Kwa Ajili ya Afrika amesema katika hotuba yake kwenye mkutano huo kwamba, ukosefu wa amani unaotokana na ugaidi unakwamisha uwekezaji vitega uchumi barani Afrika. Aidha Lopez ametaka nchi tatu zilizokumbwa na Ebola za Liberia, Sierra Leone na Guinea Conakry zifutuwe madeni.

No comments:

Post a Comment