Tuesday, January 27, 2015

DRC yatinga robo fainali AFCON


Wachezaji wa DRC

JAMHURI  ya Kidemokrasia ya Kongo imekuwa timu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kusonga hatua ya hatua ya robo fainali ya michuano Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kutoka sare ya goli moja kwa moja na Tunisia.

Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesonga mbele baada ya kumaliza ikiwa ya pili kwenye kundi B nyuma ya Tunisia ambayo nayo pia imesonga mbele ikiwa ndio inayoongoza kundi hilo.
Pamoja na kwamba imemaliza ikiwa na pointi sawa na Cape Verde idadi kubwa ya magoli iliyofungwa ndio iliyowavukisha.
Goli la pekee la Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambalo ndilo lililowavukisha kusonga mbele lilifungwa na Jeremy Bokila. Na lile la Tunisia lilifungwa na Ahmed Akaichi.

No comments:

Post a Comment