Tuesday, February 17, 2015

MORSI na wanachama wa Ikhwanul Muslimin wafunguliwa mashitaka



Mohamed Morsi

WAENDESHA  mashtaka wa kijeshi wa Misri wamewarejesha Rais wa nchi hiyo aliyepinduliwa na jeshi Mohamed Morsi na wanachama wa Harakati ya Ikhwanul Muslimin wanaokaribia 200 katika mahakama ya kijeshi ili kujibu tuhuma zinazowakabili za kuchochea mauaji.

Mmoja wa waendesha  mashtaka ya Misri ameeleza kuwa, kesi mpya itafunguliwa tarehe 23 mwezi huu.
 Kesi hiyo inahusiana na maandamano ya fujo yaliyotokea katika mji wa Mfereji wa Suez Agosti 14 mwaka juzi, kufuatia kuondolewa madarakani Rais halali wa Misri Mohamed Morsi, ambaye anatuhumiwa kuwa alichochea maandamanao hayo ya Wamisri yaliyosababisha watu 31 kupoteza maisha.
 Shirika la habari la Misri MENA limeripoti kuwa, wanachama 198 wa Ikhwanul Muslimin pamoja na kiongozi wa kundi hilo Mohamed Badie pia watapaswa kujibu tuhuma zinazowakabili mbele ya jaji wa kijeshi. Ni vyema kuashiria hapa kuwa, mahakama za kijeshi za Misri ni maarufu kwa utoaji adhabu kali.

No comments:

Post a Comment