Tuesday, February 17, 2015

WAZIRI LUKUVI na ujumbe wake watembelea Singapore


Waziri wa Ardhi akiwa na ujumbe wake pamoja na watendaji wa bodi ya nyumba nchini Sngapore

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Makazi WilliamVangimembe Lukuvi na ujumbe wake jana uliwasili nchini  Singapore kwa  Ziara ya kujifunza.


Lengo la ziara hiyo ni kwenda kujifunza namna  Serikali ya Singapore inavyoratibu upatikanaji wa nyumba kwa wananchi.

Waziri Lukuvi akiwa na ujumbe wake walitembelea Bodi ya Maendeleo ya Nyumba ya Singapore ambayo ina mamlaka ya juu ya uratibu wa masuala ya nyumba.

Bodi hiyo ya nchini Singapore imeshajenga jumla ya nyumba laki tisa mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment