Tuesday, March 17, 2015

AGONGWA na Treni na kufariki dunia



MTU mmoja asiyefahamika jina mwenye jinsia ya kiume anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka(35) hadi arobaini amefariki dunia baada ya kugongwa na treni katika eneo la Kingolwira manispaa ya Morogoro.

Wakizungumza na kituo hiki wananchi walioshuhudia tukio hilo  akiwemo mwenyekiti wa mtaa wa ujenzi Christopher Charles Chizza  na wananchi Aloyce mdoe  wameelezea kuhusiana na ajali hiyo .
Hata mwenyekiti wa mtaa huo ambao tukio hilo limetokea amesema wao  wamepata taarifa  ya kutokea ajali hiyo  majira ya asubuhi  kupitia  kwa wananchi ambao wanatumia njia hiyo  ambapo amewataka wananchi kutofanya vitendo vya kikatili kwa binadamu na kuwatupa relini kwa visingizio vya kugonjwa na tren.
Kwa upande wake  mkuu wa stesheni ya Reli Morogoro ya TRL  Bwana  Flavian Nyawale Mukoba ameelezea kuhusiana na ajali hiyo  ambapo pia  ametoa wito kwa wananchi  hususan  wanaotembea kwa miguu au usafiri wa pikipiki na baiskeli kuwa waangalifu wanapotembea  kwenye reli hiyo  kwa ajili ya usalama wao.
Mwili wa marehemu huyo  umechukuliwa jeshi la polisi mkoani morogoro  kwenda umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya rufaa mkoa wa morogoro kwa ajili ya kutambuliwa na ndugu  zake.




No comments:

Post a Comment