Tuesday, March 17, 2015

UCHAGUZI CWT mkoa wa Morogoro waaanza leo


Jengo la CWT Morogoro

KIVUMBI cha kupata viongozi wapya watakao kiongoza chama cha waalimu CWT nchini kwa miaka mitano ijayo kinaanza kutimuka leo(Mach 18) kwa chama hicho Manispaa ya Morogoro kufanya uchaguzi wake ambapo zaidi ya wanachama 100 wamejitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi mjini humo.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini ofisini kwake,katibu wa CWT mjini humo,Raphael Maswi alisema maadalizi yamekamika akiainisha kuwa karibu jumla ya nafasi 15 zitagombewa na waombaji wa nafasi hizo.

"nafasi zinazogombewa na zinaonyesha kuwa na ushindani mkubwa ngazi ya wilaya ukiacha ya katibu alieajiliwa na chama ni pamoja na Mwenyekiti inayopwaniwa na watu nane pia Mwekahazina watu nane" alisema Maswi.

Mbali na nafasi hizo pia nafasi nyingine waniwa ni mwakilishi kitengo-Ke,Walemavu,vijana,Utawala, Mahitaji maalumu,wakilishi wanne Shule za msingi,Awali,Sekondari,vyuo vya ualimu,vyuo vya ufundi na waliomba kamati ya utendaji.

"ni mkutano mkuu utakaokuwa na agenda moja tu ya Uchaguzi na baada ya hapo utafauatiwana uchaguzi ngazi ya mkoa ambapo hawa watakuwa wajumbe wake"aliongeza.

Aidha alisema kwa kipindi kifupi chama kimekuwa na mafanikio makubwa katika uendeshwaji wake jambo lililosababisha walimu wengi kujiunga na kufikia asilimia 98 sasa ikilinganishwa na asilimia 60 miaka mitano iliyopita.

mafanikio mengine ni kuanzishwa kwa Benki ya walimu itakayotoa mikopo kwa mashariti nafuu na kuboresha vivutio ikiwemo utoaji zawadi kwa wastaafu na uendelezaji walimu katika maendeleo na elimu.














No comments:

Post a Comment