Friday, March 20, 2015

CWT Moro, walaani walimu kujihusisha na uchangudoa


Mwalimu Rehema wa Morogoro sekondari akitoa sera katika Uchaguzi wa CWT Mkoa wa Morogoro
KATIBU wa chama cha walimu CWT mkoani Morogoro Issa Ngayama amekerwa na taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa walimu mkoani humo wamegeuka changudoa na kuwataka waliovamia taaluma hiyo kwa njaa kutafuta pori jingine badala ya kuidhalilisha.


Akizungumza kwa hasira dhidi ya taarifa hizo kwenye mkutano wa uchaguzi wa viongozi CWT Manspaa,Ngayama aliwataka walimu mkoani humo kuanza kuchunguzana tabia yakiwemo maadili na haiba ya ualimu.

“walimu wenzangu nimekelwa sana na hili na niwatake ninyi mkajitafakari huko hivi umeingia kwa wito au bahati mbaya! Kama ni kwa bahati mbaya niwatake mkatafute pori linguine sio kuvamia fani hii kwani hii inamiiko yake!..ualimu ni taaluma na mfano katika maadili”alifafanua

Mbali na hilo alisema walimu wa sasa wamekuwa kituko kwa jamii kutokana na kutoheshimu mifumo ya utumishi wa kada hiyo kwa walimu kuwa vinara wa mavazi ya anjabu ajabu na kauli mbaya dhiidi ya watoto nje na madarasani.

"hivi kweli mwalimu unaingia darasani umevaa kujinzi kimebana,nguo za kulalia,kinguo kinaonyesha viungo,makalio na kauli zako kama mvutabangi hivi watoto watakuwa vipi...kumbukeni mnaaminiwa kuliko yoyote mbele za
watoto na jamii sasa katika hali kama hii mnaweza kuitwa hivyo"alisisitiza.

Katika uchaguzi huo uliohudhuliwa na Afisa utumishi na utawala cwt Taifa Ally Kambi, Katibu huyo wa mkoa alimtangaza mratibu elimu kata ya Chamwino Patrick Mng’ong’o alichaguliwa kwa kura 72 dhiidi ya kura 95 kuwa mwenyekiti cwt manspaa kwa miaka Mitano ijayo.

Mbali na Patrick kuwabwaga wenzie saba pia Ngayama aliwatangaza wengine kura kwenye mabano Novatus Mzaga(81) aliewabwaga watu saba dhiidi, mwakilishi kitengo ‘ke’ shule ya msingi Jane shoo (46),mwakilishi ‘ke’ sekondari Elizabeth Werema kwa kura (70)

Kwa mujibu wa msimamizi huyo mwakilishi vijana walemavu alichaguliwa Agnes Mbaga(46),Mwakilishi walimu wa vyuo Francisca Chilongozi(48), wawakilishi wanne shule za msingi Gaston Lyuma,Hildegarda Kimotuo,Mary Mlewa na Mloka Karoli,



2 comments:

  1. Uchangudoa upo idara zote, siyo walimu pekee, lakini nguvu ya pamoja inahitajika kuondoa tatizo.Juma Salumu wa Mzumbe, Morogoro

    ReplyDelete
  2. Uchangudoa ni janga la kitaifa, siku hizi kila mkoa kuna maeneo maalumya biashara ya ukahaba.Tunakwenda wapi?Lusekelo Mbangwa wa Iringa

    ReplyDelete