Friday, March 27, 2015

WAKULIMA wa ndizi Kilosa walia na soko la uhakika



Mkulima wa ndizi kijiji cha Ulaya, wilayani kilosa

WAKULIMA  wa zao la ndizi katika vijiji vya Kidodi na Ulaya wilayani Kilosa, mkoani Morogoro, wameiomba serikali wilayani humo kuwasaidia katika kuwatafutia masokoya uhakika ya zao hilo.


Wakiongea na kipindi cha Dira ya Mazingira katika vijiji hivyo, wakulima hao wamesema kuwa, bado wakulima wa zao la ndizi hawana uhakika wa kutosha kuhusu soko la ndizi,kwani wanapata tabu sana kuuza mazao kipindi cha uvunaji.

Wamesema ukosefu wa soko la uhakika ndani ya wilaya kumesababisha zao hilo liuzwe kwa bei ya chini , ambapo mkungu mmoja uuzwa kati ya shilingi elfu tatu na elfu nne.bei ambayo haiendani na gharama za uzalishaji.


No comments:

Post a Comment