Sunday, April 5, 2015

MBUNGEatoa milioni 1.750 katika michezo


.Mbunge wa Morogoro mjini Abdul Aziz Abood

MBUNGE wa Manispaa ya Morogoro Abdul Aziz Abood ametoa shilingi Mil.1.750 zitakazotolewa kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu kati ya timu 22 zinazoshiriki kombe la Ndulu Group of Companies Ltd lililoanza jana.

Abood aliahidi kiasi hicho cha zawadi kabla hajazindua michuano hiyo na kugawa vifaa vya michezo na kufafanua kuwa mshindi wa kwanza mbali na seti tatu ya jezi,kombe na mpira atatwa shilingi Mil.1.
“kwa mshindi wa pili mbali na seti mbili za jezi na mpira walizoandaliwa na mkurugenzi Castor Ndulu mimi nawaongezea shilingi 500,000 na mshindi wa tatu mbali na pea moja ya jezi basi namwongezea shilingi 250,000”alisema Abood.
Aidha aliwataka vijana kutojisahau na michezo akiwahimiza kujiandikisha katika daftari la wapigakura ili washiriki kupata viongozi wapya katika chaguzi zijazo.
Awali akimkaribisha kuzindua michezo hiyo Mkurugenzi wa kampuni hiyo Castor Ndulu alimweleza mbunge huyo kuwa kuwa dhamira ya michezo hiyo si kwa madhumuni ya kisiasa badalatake ni maanadalizi ya kuandaa klabu ya soka ya Ndulu itakayokuwa mbadala wa timu zilizo ligi kuu nchini.
“nikutahadhalishe kuwa kunabaadhi ya wanasiasa wenzio hawakutakii mema kwa vikwazo tulivyokutana navyo wakati wa kuomba kibali kwani wanadhani unataka kututumia sisi kisiasa…lakini niualifu umma kuwa mashindono haya ni ya Ndulu na si vinginevyo”alifafanua Ndulu.
Hata hivyo katibu wa soka masipaa Khafale Maharagande aliwathibitishia wanamichezo na mbunge kuwa ligi hiyo ipo kisheria baada ya waombaji kukidhi vigezo vya uandaaji mashindano kama hayo.
Alizitaja timu zitakazo minyana katika uwanja wa Ndetembya-Kihonda kuwa ni Lamasia,Mgudeni,Eagle,Juhudi,Mlunda,Top Site,Lukobe B,Majengo,Jakalanda,Lukobe A,Muungano,Uwanja wa Taifa,Tushikamane,Uwanja waTaifa,Manyuki,Blak stone,Maduka 10,Digidigi,Ndetembia,Kilongo,Palupalu na Maendeleo.


No comments:

Post a Comment