Tuesday, June 30, 2015

SERIKALI yaombwa kuzisaidia Taasisi za mazingira katika Fukwe za Bahari ya Hindi



UHABA wa fedha kwa Taasisi zisizo za kiserikali zinazojishughulisha na Utunzaji na uhifadhi wa mazingira katika Fukwe za Bahari ya Hindi ni moja ya mambo yanayochangia uharibifu wa mazingira katika Fukwe hizo.

Hayo yamebainishwa leo na Muikolojia  na kiongozi wa Taasisi inayojihusisha na uhifadhi wa mazingira Ferry jijini Dar es salaam Bwana Mohamed Muhidini katika mahojiano maalum na kipindi cha Dira ya Mazingira wakati akielezea mikakati yao ya kutunza na kuhifadhi mikoko katika Fukwe za Bahari ya Hindi.

Amesema kuwa , serikali inapaswa kushirikiana kikamilifu na Taasisi na Asasi mbalimbali za Mazingira baharini, ikiwa ni pamoja na kuziwezesha kifedha na rasimali watu ili kufikia malengo.

No comments:

Post a Comment