![]() |
| Bunge la Tanzania |
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania, jana jioni
alifunga rasmi bunge la 10 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku idadi kubwa ya wapinza wakisusia
sherehe hizo.
Wapinzani
nchini Tanzania wamesusia hotuba ya Rais Kikwete ya kuvunja bunge hilo kama
njia ya kuwaunga mkono wenzao 32 waliofukuzwa bungeni baada ya kuupinga vikali
muswada wa mafuta na gesi wakidai umewasilishwa kinyemela kwenye bunge hilo.
Wakati wa
kulifunga bunge hilo hiyo jana, Rais Jakaya Kikwete alihusisha sehemu kubwa ya
hotuba yake katika mambo aliyosema ni mafanikio ya serikali yake tangu
alipoingia Ikulu mwaka 2005. Hata hivyo amekiri kuwa ameshindwa kulifufua
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL). Ingawa wapinzani wanaendelea kulalamikia,
lakini Rais Kikwete ametoa sifa nyingi kwa Spika wa bunge hilo Anne Makinda.
Amewashukuru pia wabunge, viongozi mbalimbali wa Serikali, wananchi na chama
chake akisisitiza kuwa anaondoka madarakani akiicha Tanzania ikiwa salama. Hata
hivyo wakati wakihojiwa kuhusu utendaji kazi wa bunge hilo la 10, wabunge
mbalimbali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamekuwa na maoni
tofauti, huku baadhi yao wakisema halikuwa na mafanikio zaidi

No comments:
Post a Comment