Thursday, July 2, 2015

RAIS Kikwete kushiriki mazishi ya Chifu Kingalu

Rmadhan Ally Kingalu 
RAIS Jakaya Kikwete (2/7/15)leo anataraji kuungana na wakazi wa mkoa wa Morogoro katika mazishi ya Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 14 Ramadhan Ally Machanga Kingalu aliyefariki dunia jana katika hospitali ya Rufani Muhimbili Jijini Dar es salaam.


Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Rajabu Rutengwe,mazishi hayo yanataraji kufanyika leo saa 7 mchana baada ya sala ya Adhuhuri huku nyumbani kwake katika kijiji cha Kinole wilayani Morogoro.

Dk Rutengwe alisema Mwanabanzi wa 14 alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Shikizo la damu na kisukari kwa muda mrefu ambapo 26.6.2015 alikimbizwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Morogoro na baadae kuhamishiwa Muhimbili kwa matibabu.

"mwili wake umesafirishwa moja kwa moja kutoka jijini Dar es salaam tangu jana hadi kijijini Kinole na wageni walianza kuwasili tangu jana kijijini huko kwa mazishi"alisema

Akiwataka wanachi wa mkoani humo kuungana na ugeni wa kitaifa katika mashishi hayo, Dk Rutengwe aliwataka viongozi mbalimbali wa makampuni,mashirika,taasisi mbalimbali zikiwemo za dini na taaluma kuungana kwa pamoja katika safari hiyo ya mwisho.







No comments:

Post a Comment