Thursday, July 2, 2015

WANNE wafariki dunia kwa ajali ya Treni

Polisi wakiwa katika eneo la ajali , Kondoa wilayani  Kilosa 
WATU wanne wamefariki dunia na 31 kujeruhiwa baada ya basi aina ya Isuzu Journey T837 TM kuigonga treni ya mizigo iliyokuwa ikitoka Mkoani Morogoro kuelekea wilayani Kilosa maeneo ya Chek-line wilaya ya  Kilosa,mkoani Morogoro.


Kwa mujibu wa abilia waliuonusurika katia ajari hiyo Maurid Yahaya(35) wa kichangani,Hasan Kikudo kondakita wa basi na Martina Kabete (59)mkazi wa jijini Dar es salaam ajali hiyo ilitokea saa 1.30 asubuhi wakati wakijaribu kukatisha kwenye reli na basi hilo.

"ilikuwa asubuhi tukitokea kijiji cha Tindiga kuelekea mjini Morogoro,tulipofika eneo la Kibaoni kuna makutano na reli sasa nadhani dereva hakujua kama kuna treni inakuja tulipofika katikati ya reli ghafla treni ikatugonga na kuburuzwa...kwa haraka haraka nadhani watu kama saba wamekufa"alisema Martina.

Hata hivyo majeruhi hao waliokimbizwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Morogoro na kulazwa wodi namba 1 na 3 walisema treni hiyo ilisimama na kuwapakia majeruhi na waliokufa kisha kuwapeleka Kilosa mjini ambako walikimbizwa hospitali ya wilaya kwa huduma za kitabibu.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu kamanda wa polisi mkoani Morogoro Musa Malambo alisema ajali hiyo ilitokea eneo hilo la Kibaoni ikihusisha basi la kampuni ya Huwel kutoka Tindiga kuelekea mjini Morogoro kushindwa kusimama na kuligonga Treni.


Alisema katika ajari hiyo ilisababisha vifo vya watu wanne hapohapo waliotambuliwa kwa majina wakiwemo wanaume wawili na wanawake wawili ambao ni Salehe Ngombaiko(35),Husna(33),Sulati Mwajiri(6)na Mwajiri(35).

Akifafanua juu ya majeruhi wa ajali hiyo kaimu Kamanda  Malambo alisema kati ya majeruhi 31 watu 10 ni wanaume,15 ni wanawake ambapo 6 ni watoto na kwamba wote wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kilosa.


Katika ufafanuzi wake Kaimu kamanda huyo aliwataja madereva wa basi kuwa ni Bakari Nyange mkazi wa Kilosa na dereva wa treni No 88 U3 ilikuwa ikiendeshwa na Inea  Chipandula(48) mkazi wa Morogoro.

No comments:

Post a Comment