Thursday, July 2, 2015

WADAU wampongeza waziri wa mazingira.

Dk Binilith Mahenge(wakwanza kushoto) akiwa na  waandishi wa habari 
WADAU wa mazingira  wameipongeza hatua iliyochukuliwa na Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi (mazingira)Dk Binilith Mahenge kwa kufunga viwanda visivyozingatia kanuni na taratibu za uhifadhi na utunzaji wa mazingira .

Wakiongea na Dira ya Mazingira jijini Dar es salaam mapema leo, baadhi ya wananchi wamesema kuwa, zoezi hilo liwe endelevu ikiwa ni pamoja nakufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kulinda afya za wafanyakzi na wananchi wanaoishi jirani na viwanda.
Wamesema , hatua hiyo ya waziri anayehusika na Mazingira kufanya ziara za kustukiza na kutoa agizo la kusimamisha shughuli za uzalishaji kwa viwanda visivyozingatia sheria, kanuni na taratibu za uhifadhi wa mazingira kwa kiasi fulani zinaonesha uwajibikaji.
Hivi karibuni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Binilith Mahenge amekifungia Kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kula cha Murzal Oil Limited kwa muda usiojulikana baada ya kukaidi agizo lililotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).





No comments:

Post a Comment