Friday, July 3, 2015

SERIKALI kuendelea kuheshimu viongozi wa jadi



RAIS Jakaya Kikwete amesema serikali itaendelea kuheshimu uongozi wa jadi nchini kwakua kufanya hivyo kunaimarisha na kuiwezesha serikali kutekeleza kwa urahisi majukumu yake ya utawala.


Rais Kikwete alisema hayo juzi kwenye mazishi ya Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 14 Ramadhan Ally Machanga Kingalu yaliyofanyika nyumbani kwake chifu huyo katika kijiji cha Kinole wilayani Morogoro.

Katika salamu za lambilambi kwa wanachi wa mkoa huo wa Morogoro na wageni kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje ya nchi Rais Kikwete alisema lengo kubwa la kuendeleza ushirikiano na viongozi hao wa kijadi ni kuimalisha amani,usalama na utulivu wa nchi.

"marehemu Chifu Machanga Kingalu 14 alikuwa msaada mkubwa katika utatuzi wa migogoro mbalimbali ikiwemo ya kijamii hususani ya wakulima na wafugaji na amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mazingira hayaharibiwi akihimiza kupanda miti na kuilinda katika maeneo mengi mkoani hapa"alisema Kikwete.

Aidha aliahidi kutafutia ufumbuzi wa changamoto ya matimizi ya nyara za serikali ikiwemo matumizi ya ngozi za wanyama katika shuguli za viongozi wa jadi kote nchini ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanishi na manufaa ya taifa kwa jumla.

Sambamba na mazishi hayo rais Kikwete akiwa na Mkewe Salma Kikwete pia alishuhudia zoezi la kumsimika chifu mpya kingalu wa 15 Husein Ali Machanga ambaye ni mdogo wake marehemu Ramadhani Ali machanga Kingalu wa 14.

Baada ya kula kiapo chifu mpya kigalu wa 15 Husen Ali alimwomba Rais Kikwete kuharakisha kupatikana ufumbuzi wa machifu kupata kibali cha matumizi ya vifaa vitokanavyo na wanyama ili waweze kuwatumikia wanachi kwa faida ya taifa.

"tofauti na zamani sasa hivi viongozi wa mila tunabanuwa na sheria zilizopo na kutufanya kushindwa kutekeleza majukumu yetu ya kimila kutokana na kukosa baadhi ya vifaa vya kutumia zikiwemo ngozi za wanyama pori kama Chui,Simba,Kenge na Mamba...tunaomba kupata kibali hata kwa kiwango fulani na Muda maalumu"alisema Chifu kingalu 15.

Chifu Kingalu Mwanabanzi wa 14 Ramadhan Ally Machanga Kingalu alifariki dunia Julai mosi katika hospitali ya Rufani Muhimbili Jijini Dar es salaam akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukali na shinikizo la damu.


No comments:

Post a Comment