WALIMU walio shule za msingi
kata mpya ya Kibuko tarafa ya Mkuyuni Wilayani Morogoro wanakusudia kuachana na
kazi hiyo kisha kujishugulisha na kazi nyingine ikiwemo biashara kutokana na hofu
ya usalama wao kiafya.
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti na timu ya waandishi wa habari iliyotembelea vijiji vya kata hiyo kwa
ushirikiano na mtandao wa jinsia nchini TGNP walimu hao walisema
kinachowakatisha tamaa ni kutelekezwa vijijini humo bila huduma muhimu licha ya
huduma ya maisha wanaopambana nayo kila kukicha.
Mbali na uduni wa nyumba
hizo, waandishi walishuhudia ukosefu wa vyoo,maji na kuwalazimu walimu kutumia
muda mwingi kusaka huduma hizo huku baadhi ya familia za walimu hao
wakilazimika kuchangia choo kimoja na familia nyingine kutumia vyoo vya shule.
Walisema kwa namna moja
au nyingine wamekuwa wakiishi mazingira magumu yakiwemo ya kudhalilika jambo
linalowaathiri kisikolojia na kufifisha juhudi zao za kufuta ujinga kwa watoto
ambao ni Taifa la kesho.
Awali kwa nyakati
tufauti wenyeviti wa kamati za shule ikiwemo ya Luholole Shiwa Chalo na shule
ya msingi Kibuko Kasimu Ramadhani walieleza kusikitishwa na serikali
kushindwa kuunga mkono juhudi za wanachi katika kuboresha maendeleo hususani
katika miundombinu ya huduma ya jamii kama shule na afya.
Kata ya Kibuko ni mpya
iliyopatikana kutoka kaya na tarafa ya Mkuyuni wilayani Morogoro na inakabiliwa
na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa ofisi na nyumba za walimu,uwekezaji
holela katika madini,misitu,maji na miundombinu ya barabara kwa miaka mingi.

No comments:
Post a Comment