Wednesday, April 6, 2016

MAKAMU wa Rais kuzindua mwenge wa Uhuru Mei 18, mkoani Morogoro

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan 
MAKAMU wa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan 18 aprili anatarajiwa kuzindua mbio za mwenge wa Uhuru kwa kuuwasha katika uwanja wa Jamuhiri Mkoani Morogoro.


Hayo yamebainishwa na Mkuu mpya wa mkoa Dk. Kebwe Stephen wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa na kufafanua kuwa zaidi ya miradi 40 inataraji kupitiwa na kuzinduliwa mkoani humo.

“Maanadalizi ya uzinduzi huo yameanza kwa kuundwa kamati tisa (9) zizitakazofanikisha zoezi hilo kubwa na lenye heshima katika mkoa wetu...Jukumu kubwa la Mkoa, pamoja na majukumu  mengine tuliyopewa ni kuhamasisha ushiriki wa wananchi na wadau wengine kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo matangazo kupitia vyombo vya habar tusaidieni”alisema Dkt  Kebwe

Aidha Dkt. Kebwe  ameagiza Wakuu wa Wilaya za Mkoa  huo ,Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya, miji midogo na Manispaa, pamoja na watendaji wote wa Serikali, kuhakikisha  wanasimamia kikamilifu maandalizi ya kufanikisha mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya na Halmashauri zote pindi utakapofika katika maeneo yao.

Kwa mjibu wa mkuu huyo wa mkoa Kaulimbiu ya mbio za Mwenge huo wa Uhuru kwa mwaka huu kitaifa ni ,  “vijana ni nguvukazi ya taifa, washirikishwe na kuwezeshwa”. 


No comments:

Post a Comment