Friday, April 8, 2016

PAPA Francis achapisha mwongozo wa familia

Papa wa kanisa katoliki Francis Paulo 
KIONGOZI  wa kanisa katoliki duniani Papa Francis amechapisha mwongozo mpya kuhusu maisha ya familia ambapo anahimiza kanisa litambue zaidi uhalisia wa maisha ya siku hizi.

Mwongozo huo ume kwenye waraka aliouandika akizingatia majadiliano ya mikutano miwili ya wakuu wa kanisa hilo kuhusu sera, maarufu kama sinodi.
Waraka huo ulisubiriwa sana na waumini takriban 1.3 bilioni wa kanisa hilo duniani.
Kicha cha waraka huo ni "On Love in the Family" (Kuhusu Upendo katika Familia) na haubadilishi mafundisho ya kidini ya kanisa hilo.
Lakini unafungua njia kwa maaskofu katika kila nchi kufafanua mafundisho ya kidini ya kanisa hilo kuambatana na utamaduni wa maeneo yao, mwandishi wa BBC anayeangazia masuala ya kidini Caroline Wyatt anasema.
Papa Francis amewahimiza mapadri kutumia hekima na busara wakishughulikia “familia zilizoumizwa” na kuwa na huruma badala ya kutoa hukumu haraka.
Amekosoa ubinafsi ambao anasema umewafanya watu wengi katika nchi za magharibi kuthamini sana kutosheleza mahitaji yao binafsi badala ya mahitaji ya wake au waume zao katika ndoa.
Huku akiunga mkono kutolewa kwa elimu kuhusu ngono, amesema inafaa kuwa kwenye mfumo wa kutoa elimu kuhusu upendo.
Amesisitiza sana kuhusu ulezi wa kiroho na kuandaliwa vyema kwa watu kabla ya kufunganishwa kwenye ndoa kuhusu mahitaji ya maisha katika ndoa.





No comments:

Post a Comment