Wednesday, April 6, 2016

WATU wawili wahofiwa kufa maji mjini Morogoro

Kituo cha mabasi cha Msamvu Morogoro mjini 
WATU wawili Baba Galinus Laulent(35-38) na wanae Mariam Laulent(10 -13) mwanafunzi darasa la nne shule ya msingi Kauzeni wote wakazi wa Mzinga Manispaa ya Morogoro wanahofiwa kufa maji baada ya kusombwa na maji katika mto Mvuha kati ya kijiji cha Nemele na Baga wakati wakijaribu kuvuka kwenda msibani.

Mashuhuda wa tukio hilo juzi saa11 jioni akiwemo kaka wa marehemu Mpeka Hussen(43) na Martin Ng’humbi walisema watu hao wakitokea Kauzeni mjini Morogoro walifika Matombo na kuanza safari kwenda kijijini Baga kwa miguu kuhani msiba.
Walisema wakiwa safarini kwenda kijiji cha Singisa-Kiseli walifika kijiji cha Nemele ulipo mto huo wa Mvuha unaoatenganisha vijiji viwili cha Baga na kijiji cha Nemele kisha kuingia na kuanza kuvuka,wakati huo hapakuwa na maji mengi.
“wao walikuwa mbele akawa amembeba mwanae huyo na kuanza kuvuka, kwa jumla maji haya kuwa mengi kwa kukadiria kama nchi 15,walipofika katikati ya mtoghafla yakaongezeka nahisi waliteleza baada ya kukanyaga jiwe na kuanguka…walipoinuka wakawa hawa naguvu wakasombwa na maji” alisem Mpeka.
Alisema hata alipojaribu kuwaelekeza kuwaelekeza kushika kwenye vipande vya miti vilivyokuwa mtoni humo hawakuelewana kiasikwamba walikuwa wakizamishwa na kuibuka huku wakisukumwa na maji hayo yaliyokuwa machafumithiri ya mvua kunyesha maeneo ya juu milimani.
Kwa upande wake Ng’humbi mbali na kuelezea hayo alisema ongezeko hilo la maji lilitokana na mvua nyigi kunyesha majuzi usiku kucha katika milima ambayo mifereji na vijito vyake vinaingiza maji kwenye mto huo nakuwa inawezekana kwa





No comments:

Post a Comment