Saturday, May 21, 2016

YANGA yakonga nyoyo za mashabiki wake na watanzania kwa ujumla

wachezaji wa timu ya  Yanga wakiwa uwanja wa ndege wa Mwl Nyerere
JIJI la Dar es Salaam jana lilisimama kwa muda, wakati mabingwa wa Tanzania, Yanga walipowasili wakitokea Angola walikofuzu hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF CC).


Mamia ya mashabiki wa Yanga walianza kumiminika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam kuanzia saa tano asubuhi na hadi kufikia saa nane mchana hali uwanjani hapo ilikuwa si ya kawaida.
Pia mashabiki wa Yanga walijipanga barabarani katika maeneo mbalimbali kuanzia Uwanja wa Ndege, Kipawa, Vingunguti na Tazara, ambapo mara kadhaa msafara wa basi la wachezaji wa Yanga uliokuwa ukiongozwa na bodaboda kadhaa ulilazimika kusimama mara kwa mara sababu ya mashabiki walikuwa wanataka kuwaona.
Kivutio kikubwa katika mapokezi hayo alikuwa kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ aliyepangua penalti ya dakika ya 90, ambaye mashabiki walikuwa wakimgombea kutaka kumbeba.


No comments:

Post a Comment