![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Morogoro Kebwe Stevenm Kebwe |
SERIKALI mkoani Morogoro
imeziagiza shule zote za sekondari mkoni humo kuelekeza nguvu katika masomo ya
sayansi kwa wanafunzi wake ikiwa ni mkakati wake kuzalisha rasilimali
watu ili mkoa huo ulikabili soko la ajira kutokana na sera iliyopo
ya Tanzania ya sasa ni ya viwanda.
Wito huo umetolewa na
Mkuu wa Mkoa huo Dk.Kebwe Stephen Kebwe wakati akiwahimiza walimu na wanafunzi
wa shule za sekondari Lubeho wilayani Gairo na kusisitiza kuwa bila kuwa na
wataalamu wakiwemo wa ipo hatari dhana ya viwanda ikakosa mantiki
iliyokusudiwa.
Alisema mkoa wa Morogoro
umewekwa kama dira ya utekelezwaja sera hiyo ambapo ili ikamilike
lazima wanachi,walimu na wanafunzi kushirikiana kwa dhati ili kuwe na wataalamu
mahususi watakao mudu teknolojia mpya inayohitaji uelewa wa sayansi.
“wazazi inatupasa
kuwaboreshea watoto mazingira ya kusomea kama kuhakikisha madawati,vyumba vya
madarasa na maabara vinakuwepo kuhuku walimu mkitakiwa kujitahidi kuwaelimisha
watoto kwa bidii nao watoto kuwa wadadisi zaidi ili tupate wanasayansi bora”
alisema Mkuu huyo wa mkoa.
Dk Kebwe amabye
alilazimika kisitisha msafara wake kwa muda kuzungumza na wanachi walikuwa
wamefurika shule ya sekondari ya Lubeho wakati akikagua vyumba vya
madarasa,maabara na samani alisema endapo fulsa hiyo itachezewa na wanachi
mkoani humo wasishangae kuwanufaisha wengine.
Aliwataka wanafunzi
kusoma ya mchepuo wa Sayansi na kuyapenda masomo hayo likiwemo somo la
Baiolojia, fizikia na kemia kwa kuwa ni rahisi isipokuwa uvivu wa wanafunzi ndi
umekuwa chanzo cha kuyachukia na kuyakimbia.
“Masomo ya sayansi sio
magumu kama wengine wanavyosema, ni masomo rahisi sana kuliko masomo mengine
kama biashara na sanaa lakini pia sayansi ni maisha yetu tunayoishi nayo kila
kukicha” alisema Dk.Kebwe.
Aidha, aliwataka
wanafunzi kupenda michezo kwa ajili ya kuuweka mwili kuwa mkakamavu wenye Afya
hali itakayopelekea kiakili kufanya kazi kwa wepesi lakini pia kuongeza
mahusiano mazuri baina ya wanafunzi hata walimu wao kupitia michezo.
Kwa upande wa
madawati, Mkuu huyo wa Mkoa aliutaka uongozi wa Wilaya ya
Gairo kusimamia suala nzima la ubora wa madawati yanayotengenezwa na kuagiza
kuitisha kongamano la wadau wa Elimu wilayani humo ili kutafakari namna
watakavyotekeleza agizo la Rais kabla ya Juni 30.
Hadi mwanzoni mwa mwezi
Juni Wilaya ya Gairo ilikuwa inakabiliwa na upungufu wa samani 7,229 ikiwa ni
pamoja na meza 960, viti 1,127 na madawati 5,142 samani ambazo hadi
kukamilika kwake zitagharimu karibu shilingi 307 milioni.

No comments:
Post a Comment